Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tetesi za soka Jumapili:Bayern Munich wanavutiwa na Rogers wa Aston Villa
Morgan Rogers wa Aston Villa analengwa na Bayern Munich, ambao wamejiunga na Chelsea na Manchester United katika kumtaka mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 23. (Football Insider)
Kiungo wa kati wa Uingereza Curtis Jones, 25, anajiandaa kuondoka Liverpool msimu huu wa joto, huku Aston Villa ikiwa tayari mbioni kumnyakua. (Teamtalk)
Manchester City inaendelea kuweka kipaumbele katika uhamisho wa mlinzi wa Newcastle United wa Uingereza Tino Livramento, 23, lakini pia wanatafuta mbadala. (Teamtalk)
Real Madrid wanafikiria kumteua meneja wa zamani Jose Mourinho, ambaye yuko Benfica. (Record)
Real Madrid itafanya uamuzi kuhusu mustakabali wa meneja Alvaro Arbeloa mwishoni mwa msimu. (Marca)
Real Madrid wanapanga kufanya marekebisho makubwa ya kikosi chao msimu huu wa joto, huku kiungo wa kati wa Ufaransa, Eduardo Camavinga, 23, akiondoka. (Sport )
Kupandishwa kwa Coventry City hadi Ligi Kuu kunamaanisha uhamisho wa mkopo wa kiungo wa Nigeria Frank Onyeka, 28, kutoka Brentford utakuwa wa kudumu. (Talksport)
Lorient wanamfikiria aliyekuwa kocha wa Lens na Southampton Will Still kama chaguo la nafasi ya meneja. (L'Equipe)