Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
UEFA-Mfumo mpya wa Upigaji wa Mikwaju ya Penalti
Shirikiksho la kandanda barani Ulaya UEFA Lipo katika mikakati ya kufanya majaribio mfumo mpya wa upigaji wa mikwaju ya Penalti mitano mitano ili kuondoa faida ya timu inayoanza kupiga Penalti hizo.
Mfumo huo mpya, ambao unatambuliwa kama ABBA, utatumika kwa timu ya kwanza itayotambulika kama timu A kupiga penalti ya kwanza na kisha timu B kupiga penalti ya pili na ya tatu na kisha timu B kupiga penalti ya nne na ikifuatia zamu ya timu A kupiga Penalti ya 5 na ya 6 kwa kupokezana hivyo kila moja kukamilisha Penati 5.
Mfumo huo umependekezwa na IFAB ambacho ni chombo pekee chenye mamlaka ya kubadili sheria za soka.