Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh ameshinda uchaguzi uliosusiwa na upinzani, baada ya kupata zaidi ya asilimia 97.81 ya kura zilizopigwa, data rasmi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani Jumamosi ilionyesha.
Kura ya Ijumaa ilimkutanisha mpinzani mmoja pekee na aliyemaliza muda wake, Mohamed Farah Samatar. Takwimu za Wizara ya Mambo ya Ndani zilionyesha kuwa aliibuka wa pili kwa 2.19% ya kura 168,233 zilizopigwa.
Guelleh alishinda uchaguzi uliopita wa 2021, ambao pia uliosusiwa na wagombea wengi wa upinzani, kwa zaidi ya 97% ya kura.
Alikuwa ametangaza kujiuzulu mwaka huu, lakini marekebisho ya katiba mwezi Novemba yaliondoa ukomo wa umri wa juu wa miaka 75 kwa wagombea urais.
Wakosoaji wamepuuza matokeo ya uchaguzi huo wakisema haukua na ushindani, huku wafuasi wakihoji kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 78 ameleta utulivu katika taifa hilo la kimkakati la Pembe ya Afrika.
Mpinzani maarufu Daher Ahmed aliiambia BBC kwamba wanasusia uchaguzi nchini Djibouti kwa sababu hawaruhusiwi kuwa na uchaguzi huru na wa haki, jambo ambalo wanaamini linadhoofisha mchakato wa kidemokrasia na uhalali wa matokeo ya uchaguzi.
Kampeni ya Rais Ismail Omar Gelleh ilijikita zaidi katika kuleta utulivu huku kukiwa na mvutano wa kikanda, hasa unaohusishwa na migogoro katika Mashariki ya Kati, wakati Samatar amejikita katika mageuzi ya kiuchumi na elimu.
Rais huyo amekuwa madarakani tangu mwaka 1999 na ndiye rais wa pili wa nchi hiyo tangu ilipojipatia uhuru wake kutoka kwa Ufaransa mwaka 1977.