Lebanon yatilia shaka madai ya mazungumzo ya Trump
Afisa katika ofisi ya rais wa Lebanon ameiambia BBC kuwa nchi hiyo haina taarifa yoyote kuhusu mawasiliano yajayo na Israel, kufuatia ujumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump uliodokeza uwezekano wa mazungumzo kati ya viongozi wa mataifa hayo mawili.
Trump alisema usiku uliopita kuwa mazungumzo kati ya viongozi wa Israel na Lebanon yanatarajiwa kufanyika “leo”.
Siku ya Jumanne, maafisa wa Israel na Lebanon walifanya mazungumzo mjini Washington, D.C., ikiwa ni mara ya kwanza kwa pande hizo kufanya mazungumzo ya moja kwa moja tangu mwaka 1993.
Lebanon ilielezea mazungumzo hayo kuwa “yenye tija”, huku Israel ikisema kuwa pande zote ziko “upande mmoja wa mlinganyo”, ingawa mashambulizi ya Israel dhidi ya kundi la Hezbollah yanaendelea.