Idara ya Hazina ya Marekani yatangaza vikwazo vipya dhidi ya Iran

Chanzo cha picha, Reuters
Idara ya Hazina ya Marekani imetangaza mfululizo mpya wa vikwazo dhidi ya watu binafsi, mashirika na meli zinazohusishwa na Iran.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya idara hiyo, vikwazo vimewekwa dhidi ya watu watatu, meli tisa na taasisi 17, ambapo neno “taasisi” linaweza kujumuisha kampuni au mashirika mbalimbali.
Katika taarifa yake, Idara ya Hazina ya Marekani imesema imeweka vikwazo dhidi ya mtandao wa usafirishaji mafuta unaoendeshwa na Mohammad Hossein Shamkhani, mtoto wa afisa wa zamani wa usalama wa Iran Ali Shamkhani.
Anatuhumiwa kuhusika katika usafirishaji na uuzaji wa mafuta ya Iran kupitia mtandao mpana wa majini.
Kwa mujibu wa maafisa wa Marekani, mtandao huo umeingiza mapato ya mabilioni ya dola.
Idara hiyo pia imeweka vikwazo dhidi ya malengo yanayohusishwa na mpango tata wa kifedha unaohusishwa na kundi la Lebanon la Hezbollah, unaodaiwa kupangwa kupitia vituo vya kubadilisha dhahabu na hatimaye kunufaisha utawala wa kijeshi wa Iran.
Kwa mujibu wa maafisa wa Marekani, mpango huo unahusisha kubadilisha akiba ya dhahabu kuwa fedha taslimu, ambazo hutumika kufadhili shughuli za Hezbollah huku ukikwepa vikwazo kupitia mitandao ya biashara na usambazaji.
Soma zaidi:




