Mashirika ya ndege Ulaya yaonya uhaba wa mafuta Mlango wa Bahari wa Hormuz usipofunguliwa
Ulaya huenda ikakabiliwa na uhaba wa mafuta ya ndege ikiwa Mlango wa Bahari wa Hormuz hautafunguliwa katika kipindi cha wiki tatu zijazo, kulingana na shirika la biashara la viwanja vya ndege vya Ulaya.
ACI Ulaya imewaandikia Makamishna wa Uropa wa nishati na utalii, ikionya juu ya "kuongezeka kwa wasiwasi" kati ya wanachama wake kuhusu upatikanaji wa mafuta ya ndege.
"Kupungua kwa usambazaji kunaweza kutatiza sana shughuli za usafiri wa anga - na hii itasababisha athari mbaya za kiuchumi kwa jamii zilizoathirika, na kwa bara Ulaya," mkurugenzi mkuu wa ACI Barani Ulaya aliandika.
"Katika hatua hii, tunaelewa kwamba ikiwa njia ya kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz haitafunguliwa ndani ya wiki tatu zijazo, Umoja wAa Ulaya utakumbwa na uhaba wa mafuta."
Nchi za Ghuba ni chanzo kikuu cha mafuta ya ndege, zikisafirisha takriban 50% ya bidhaa zinazoagizwa kutoka Ulaya.
Mashirika kadhaa ya ndege tayari yamepunguza safari za ndege na kuongeza gharama za usafiri kwa abiria kutokana na wasiwasi kuhusu uhaba wa mafuta.
Wiki iliyopita, bei ya mafuta ya ndege ya Ulaya ilifikia kiwango cha juu kabisa cha dola 1,838 za Kimarekani kwa tani, ikilinganishwa na dola 831 kabla ya vita kuanza.
Soma zaidi: