Lazima tulipize kisasi kifo cha Ali Khamenei - Mojtaba Khamenei
Kiongozi Mkuu wa Iran,Mojtaba Khamenei, amesema kuwa lazima walipize kisasi kifo cha baba yake, Ali Khamenei, akisema hayo ni "matakwa ya taifa" na "lazima yatimizwe."
Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa Telegram, baada ya kukamilika kwa mazishi ya babake aliyekuwa kiongozi wa awali wa Iran, Ali Khamenei.
Taarifa ya Mojtaba ilisema kuwa:
"Tunaahidi kulipiza kisasi damu ya kiongozi shahidi mashahidi wote wa vita hivi, kutoka kwa wauaji na wahalifu waliomvunjia heshima."
Mojtaba Khamenei, ambaye alichukua nafasi ya Kiongozi Mkuu wa Iran baada ya kifo cha baba yake, hakuhudhuria mazishi ya baba yake.
Soma pia: