Iran na Oman kujadili kuhusu usalama wa Mlango bahari wa Hormuz

Chanzo cha picha, ISNA
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran, Abbas Araqchi, amewasili mjini Muscat, Oman, kwa mazungumzo na maafisa wa serikali ya Oman.
Kulingana na vymbo vya habari vya eneo hilo, Waziri huyo anatarajiwa kuongoza mazungumzo kati ya Iran na Oman kuhusu mlango bahari wa Hormuz
Pande hizo mbili zinatarajiwa kuja na utaratibu utakaohakikisha meli zinapita kwa usalama katika Mlango wa Bahari wa Hormuz, kwa kuzingatia Kifungu cha 5 cha Hati ya Makubaliano ya Islamabad.
Ziara hiyo inafanyika wakati mvutano kuhusu Mlango Bahari wa Hormuz umeongezeka katika siku za hivi karibuni kufuatia mashambulizi kati ya Marekani na Iran.
Hayo yakijiri, ujumbe wa wapatanishi kutoka Qatar umesafiri kwenda Iran kwa lengo la kuweka mazingira ya kuanza tena mazungumzo kati ya Iran na Marekani pamoja na kupunguza mvutano kati ya pande hizo mbili.
Soma pia:




