Tetesi za soka Ulaya Alhamisi: Man Utd yamtupia jicho Summerville

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Winga wa West Ham Crysencio Summerville, anawindwa na Manchester United. Arsenal wanajiandaa kuwasilisha ofa kwa winga wa Norway, Antonio Nusa, huku Everton wakifikiria kumsajili Rico Lewis wa Manchester City.

Manchester United watamlenga winga wa West Ham Crysencio Summerville, mwenye umri wa miaka 24, iwapo Marcus Rashford ataondoka msimu huu wa kiangazi. Mshambuliaji huyo wa Uholanzi anakadiriwa kugharimu takriban pauni milioni 30. (Guardian - subscription required)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Arsenal wanajiandaa kuwasilisha ofa ya takribani pauni milioni 34 kwa winga wa Norway mwenye umri wa miaka 21, Antonio Nusa, kutoka RB Leipzig. (CaughtOffside)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Manchester City wamefahamisha Lille kwamba wanataka kumleta kiungo wa Morocco mwenye umri wa miaka 18, Ayyoub Bouaddi, moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza badala ya kumrudisha kwa mkopo katika klabu hiyo ya Ufaransa. (TeamTalk)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Manchester City wanamfuatilia mshambuliaji wa Senegal mwenye umri wa miaka 18, Ibrahim Mbaye, wa Paris Saint-Germain, huku Aston Villa na Tottenham pia wakimwania. (FootMercato)

Sunderland wanajiandaa kuwasilisha ofa ya kumsajili beki wa Ufaransa,19, Dayann Methalie, kutoka Toulouse. (Football Insider)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Everton wanafikiria kumsajili beki wa kulia wa Manchester City, Rico Lewis, huku Nottingham Forest, Bournemouth na Fulham pia zikimwania Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 21. (TeamTalk)

Hull City wanatarajiwa kukamilisha usajili wa winga wa Sweden mwenye umri wa miaka 24, Elliot Stroud, kutoka Mjallby katika dili la pauni milioni 3 wiki hii. Pia wana matumaini ya kukamilisha usajili wa kipa wa Olympiacos na timu ya taifa ya Ugiriki, Konstantinos Tzolakis, mwenye umri wa miaka 23. (Sky Sports)