Kesi ya pamoja ya washukiwa 486 wa magenge ya uhalifu yaanza El Salvador

Chanzo cha picha, Getty Images
Kesi ya pamoja dhidi ya washukiwa 486 wanaodhaniwa kuwa wanachama wa genge la MS-13 imeanza nchini El Salvador, ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo imesema.
Picha zilizotolewa na ofisi hiyo zinaonyesha makundi makubwa ya wanaume walioko gerezani wakishiriki kesi hiyo kupitia muunganisho wa video.
Kundi hilo linatuhumiwa kwa pamoja kufanya zaidi ya uhalifu 47,000, ikiwemo mauaji, uhalifu wa kulazimisha watu kutoa fedha, na usafirishaji wa dawa za kulevya na silaha kati ya mwaka 2012 na 2022.
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanasema kesi za aina hii za pamoja “hudhoofisha haki ya utetezi na dhana ya kutokuwa na hatia kwa washtakiwa.”
Hata hivyo, ofisi ya Mwanasheria Mkuu imesema ina ushahidi “wa kutosha” utakaowezesha kutolewa kwa “adhabu kali zaidi” kwa watakaopatikana na hatia.
Soma zaidi:












