Iran yasema imekamata meli mbili Hormuz baada ya meli tatu kushambuliwa
Vyombo vya habari vya Iran, ikiwemo kituo cha Telegram cha televisheni ya taifa ya Iran, vimechapisha taarifa ya Jeshi la Wanamaji la Islamic Revolutionary Guard Corps.
Katika taarifa hiyo, Jeshi la Wanamaji la IRGC linasema kuwa meli mbili, MSC Francesca na Epaminondas, zimepelekwa katika maji ya Iran kwa ajili ya “ukaguzi wa mizigo, nyaraka na vitambulisho vyao.”
Inadai kuwa meli hizo zilikuwa “zinafanya kazi bila idhini” na zilifanya “ukiukaji mara kadhaa,” huku zikishutumiwa kujaribu kuondoka katika Mlango wa Bahari wa Hormuz “kwa siri”.
Shirika la BBC halijaweza kuthibitisha kwa kujitegemea madai hayo.
Jeshi la Wanamaji la IRGC pia limeonya kuwa linafuatilia kwa karibu shughuli zinazoendelea katika mlango huo wa kimkakati wa Hormuz na limeapa kuchukua hatua kali dhidi ya wanaokiuka sheria.
Katika taarifa hiyo hakukutajwa meli ya Euphoria, ambayo iliripotiwa awali kushambuliwa pia siku ya Jumatano.
Unaweza pia Kusoma: