Trump amesema Marekani inafanya kazi kwa karibu na Iran

Trump anasema Iran haitarutubisha urani, na Marekani itashirikiana na Tehran "kuchimba na kuondoa 'chembechembe' zote za Nyuklia.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Madagascar yatangaza hali ya dharura kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta unaohusishwa na vita vya Iran

    Mafuta

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Madagascar imetangaza hali ya dharura kwa muda wa wiki mbili kufuatia uhaba mkubwa wa mafuta uliosababishwa na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

    Mamlaka zimesema uamuzi huo ulifikiwa baada ya kikao cha baraza la mawaziri Jumanne, kutokana na hofu kwamba hali hiyo inaweza kusababisha vurugu za kijamii.

    Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi, ambacho hutegemea mafuta kuzalisha sehemu kubwa ya umeme wake, kinategemea uagizaji wa mafuta kutoka Mashariki ya Kati na usambazaji unatarajiwa kuathirika kwa muda, licha ya kusitishwa kwa mapigano kwa wiki mbili kulikotangazwa usiku.

    Mwaka jana, kukatika kwa mara kwa mara kwa umeme na maji nchini Madagascar kulisababisha maandamano yaliyoongozwa na vijana, ambayo baadaye yaligeuka kuwa machafuko ya kisiasa na kusababisha jeshi kuchukua madaraka.

    Haijulikani wazi hatua mahsusi ambazo serikali inapanga kuchukua, lakini imesema sasa ina mamlaka ya kuimarisha sekta ya umeme, kupunguza usumbufu zaidi, kudhibiti matumizi, na kuhakikisha huduma za umma zinaendelea.

    Unaweza kusoma;

  2. Falme za kiarabu “ilishinda” vita hivyo

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Mshauri wa rais wa Falme za Kiarabu amesema kuwa taifa hilo “lilipata ushindi” baada ya kushambuliwa mara kadhaa na Iran tangu kuanza kwa vita hivyo.

    “Tulishinda kupitia ulinzi wa kitaifa wa kihistoria uliolinda uhuru, heshima, na kutunza mafanikio yetu baada ya kuchokozwa,” alisema Anwar Gargash.

    “Leo, tunasonga mbele tukikabiliana na mazingira magumu kwenye ukanda wetu tukiwa na nguvu zaidi, uelewa zaidi, na uwezo thabiti wa kushawishi mustakabali wa siku za usoni.”

    Wizara ya ulinzi ya taifa hilo imekuwa ikichapisha taarifa ya jinsi imekuwa ikidungua makombora ya Iran.

    Hapo jana katika taarifa waliyoitoa, tangu kuanza kwa vita hivyo wameweza kudundua ndege zisizo na rubani 2221, makombora ya majini 26 na makombora ya kibalistiki 520.

    Waziri wa mambo ya kigeni wa Oman, ameipongeza Pakistan kwa juhudi zao za kuhakikisha mkataba huo unaafikiwa na kusema kuwa anatumai utakuwa wa kudumu.

    Pia unaweza kusoma;

  3. Wairani wakusanyika mjini Tehran baada ya tangazo la kusitishwa mapigano

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Raia wa Iran wamekusanyika katika mji mkuu wa taifa hilo, Tehran, wakiwa wamebeba bendera ya taifa na mabango yenye picha ya Kiongozi Mkuu Mojtaba Khamenei.

    Raia wa Iran wamejitokeza katika barabara za mji wa Tehran baada ya kutangazwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa muda.

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Kusitishwa kwa vita hivyo kwa muda kumepokelewa kwa hisia mseto miongoni mwa raia wa Iran.

    Kuna afueni kwa sababu viwanda vya nishati havitashambuliwa tena, lakini kwa wale ambao wanapinga utawala wa taifa hilo, hawajalipokea vyema.

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Soma zaidi:

  4. Israel yaunga mkono rasmi usitishaji mapigano lakini 'haujumuishi Lebanon'

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Israel imetoa taarifa rasmi kuhusu kusitisha mapigano na Iran.

    Hii hapa kamili:

    Chapisho kamili:

    Israel inaunga mkono uamuzi wa Rais Trump wa kusimamisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa wiki mbili ikiwa Iran itafungua mara moja Mlango Bahari na kusimamisha mashambulizi yote dhidi ya Marekani, Israel na katika nchi za eneo hilo.

    Israeli pia inaunga mkono juhudi za Marekani kuhakikisha kwamba Iran sio tena tishio la nyuklia, kombora na ugaidi kwa Marekani, Israeli, majirani wa Kiarabu wa Iran na ulimwengu.

    Marekani imeiambia Israeli kwamba imejitolea kufikia malengo haya, ambayo pia ni ya Marekani, Israeli na washirika wa kikanda wa Israeli, katika mazungumzo yajayo.

    Usitishaji mapigano wa wiki mbili haujumuishi Lebanon.

    • Katika muktadha: Hapo awali, Waziri Mkuu wa Pakistani Shehbaz Sharif alisema kusitisha mapigano kulihusisha Lebanon.

    Soma zaidi: