Trump asema atasitisha mashambulizi baada ya ombi la Iran
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa mashambulizi dhidi ya Iran "yataisha hivi karibuni" baada ya ombi kutoka Iran.
Kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Fox News Trump alisema katika mahojiano kwamba aliamuru kusitishwa kwa mashambulizi mapya dhidi ya Iran baada ya kupokea "simu ya moja kwa moja kutoka Iran" na ombi kutoka kwa afisa mwandamizi wa Iran.
Hata hivyo, vyombo vya habari rasmi vinavyohusishwa kwa karibu na jeshi la mapinduzi ya Iran vimekanusha madai hayo hadharani, vikisema kuwa ni "uongo" kwamba Iran iliomba mashambulizi hayo yasitishwe.
Mwandishi wa Fox News pia alisema kuwa Trump alieleza katika mahojiano hayo kwamba mashambulizi yaliyofanyika ndani ya Iran yalihusisha makombora ya aina ya Tomahawk, yaliyolenga rada za ulinzi, vituo vya ulinzi na mifumo ya kuongozea ndege zisizo na rubani za Iran.
Mashambulizi hayo yanaripotiwa kufanyika ndani ya Iran, kilomita chache kutoka mji mkuu, Tehran.
Alipoulizwa kuhusu uwezekano wa Iran kukataa makubaliano yaliyopendekezwa na Marekani, Trump alijibu:
"Iwapo watafanya hivyo, watashambuliwa tena kwa mabomu."
Kauli hizi zinaonesha kuendelea kwa mvutano mkubwa kati ya Marekani na Iran, huku pande zote zikitoa taarifa zinazokinzana kuhusu mawasiliano na juhudi za kusitisha mashambulizi.
Unaweza kusoma;