Moja kwa moja, Mjumbe wa Trump akutana na kiongozi wa Hamas kushinikiza mpango wa amani Gaza

Afisa mmoja wa Palestina ameiambia BBC kuwa mkwe wa Trump alikutana na ujumbe ulioongozwa na kiongozi mpya wa Hamas, Khalil al-Hayya, nchini Misri siku ya Jumapili.

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Iran yatangaza zawadi nono kwa atakayemua au kumkamata mwanajeshi wa Marekani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kamanda wa Jeshi la Iran, Amir Hatami, ametangaza kuwa yeyote atakayemuua au kumkamata mwanajeshi wa Marekani na kumkabidhi kwa mamlaka atapewa zawadi ya dola 30,000; lakini ikiwa mwanamke atafanya hivyo, zawadi hiyo itaongezwa maradufu.

    Kulingana na ripoti ya shirika la habari la serikali ya Iran (IRNA), Hatami alisema uamuzi huo umefikiwa kufuatia maombi mengi kutoka kwa wananchi waliotaka kuchangia fedha za zawadi hiyo.

    "Jeshi litatoa zawadi ya dola 30,000 kwa yeyote atakayemuua au kumkamata afis wa vikosi vya Marekani, na ikiwa mwanamke atafanya hivyo, zawadi hiyo itaongezwa maradufu," IRNA ilimnukuu Hatami akisema.

    Hakutaja muda au mahali maalum ambapo mashambulizi hayo yanayoweza kutokea.

    Hakuna ripoti rasmi iliyotolewa kuhusu uwepo wa vikosi vya ardhini vya Marekani ndani ya Iran tangu kuanza kwa vita, isipokuwa tukio moja la mwezi Aprili mwaka jana la kuokelewa rubani wa ndege ya Marekani iliyoanguka.

    Kamanda huyo wa jeshi la Iran aliongeza kusema, "Uwepo wa Marekani kimsingi 'umeshafukuzwa' kutoka eneo hili na kwa mtazamo wa Tehran, vikosi vya Marekani havina tena haki ya kuingia katika Ghuba, Lango la Hormuz, na Bahari ya Oman."

  2. Korea Kusini yaanza mazoezi ya kijeshi na Marekani

    Kadhaa baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kuwa angepunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha mazoezi ya kijeshi ya nchi yake na Korea Kusini, Seoul imetangaza kuanza kwa mazoezi hayo.

    Bw. Trump alisema kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ndiye aliyemfanya kufikia uamuzi huo. Aliyataja mazoezi hayo kuwa ya gharama kubwa na ya kichokozi, huku akigusia hatua ya Korea Kusini kukataa kujiunga na mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

    Mazoezi ya 'Ulchi Freedom Shield' hufanyika kila mwaka ili kujiandaa dhidi ya tisho la mashambulizi katika Rasi ya Korea.

    Korea Kaskazini inaendelea kuimarisha silaha zake za nyuklia na wiki iliyopita ilifanya majaribio kadhaa ya makombora ya masafa marefu (ballistic missiles). .

    Katika ujumbe wake wa mitandao ya kijamii siku ya Jumapili, Trump alisema ilikuwa "ni vigumu kuahirisha," mpango huo kwani Marekani na Korea Kusini zilikuwa zikitarajiwa kuanza mazoezi yao ya kila mwaka ya kijeshi Jumatatu.

  3. Matukio ya vurugu yagubika mkutano wa 'Linda Mwananchi' Homa Bay magharibi mwa Kenya

    Sifuna

    Chanzo cha picha, Edwin Sifuna/Facebook

    Kaunti ya Homa Bay ilishuhudia hali ya wasiwasi mkubwa wa kisiasa na hofu kuhusu usalama siku ya Jumapili, tarehe 16 Agosti, wakati vuguvugu la 'Linda Mwananchi' - mrengo hasimu wa chama cha upinzani cha Orange Democratic Movement (ODM) lilipofanya mkutano mkubwa wa kisiasa huko Nyandiwa, huku kukiwa na ripoti za kufungwa kwa barabara, mapigano, uharibifu wa mali na mashambulizi dhidi ya waandishi wa habari.

    Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani hali ya wasiwasi ilianza mapema Jumapili, ambapo barabara kuu zinazoelekea maeneo ya Mji wa Homa Bay na Nyandiwa ziliripotiwa kufungwa kwa mawe makubwa na vizuizi vingine.

    Baadhi ya njia zilikuwa hazipitiki, jambo lililotatiza usafiri wakati wafuasi na viongozi wa kisiasa wakielekea kwenye mkutano huo uliopangwa.

    Msafara wa 'Linda Mwananchi' uliripotiwa kulazimika kutumia njia mbadala, ikiwemo barabara mbovu na njia za kutembea kwa miguu, ili kufika Nyandiwa baada ya sehemu za barabara kuu kufungwa.

    Maafisa wa usalama waliusindikiza msafara huo huku hali ya wasiwasi ikiongezeka katika maeneo kadhaa ya kaunti hiyo.

    Makabiliano yaliropotiwa baadaye ambapo gari moja lilichomwa moto, watu kadhaa wakiwemo waandishi wa habari kujeruhiwa, na washukiwa 17 kukamatwa.

    Kwa mujibu wa mashuhuda mashambulizi hayo yaliyodaiwa kuwalenga wafuasi wa Linda Mwananchi yalianza usiku wa Jumamosi wakati wahuni waliposhambulia hoteli moja Homa Bay; kuvunja madirisha, kuharibu mali na kuiba vitu kabla ya kuondoka kwa kutumia pikipiki.

    Walikuwa wamejihami kwa mawe na rungu walipokuwa wakipita eneo la Nyandiwa, Suba Kusini, ambapo kundi la 'Linda Mwananchi' ilikuwa imepanga kuhudhuria ibada kanisani.

    Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International Kenya, limelaani matukio hayo na kuelezea wasiwasi kuhusu vitendo vya vurugu dhidi ya waandishi wa habari, kuvurugwa kwa matangazo ya vyombo vya habari, uharibifu wa mali, uwekaji wa vizuizi visivyo halali barabarani na vitisho.

    Shirika hilo linataka uchunguzi ufanywe kubaini chanzo cha vurugu hizo na kutoa wito kwa mamlaka kulinda haki za kikatiba za raia pamoja na usalama wa umma.

    Maelezo zaidi:

  4. Trump: Ninapunguza kiwango cha mazoezi ya kijeshi ya Marekani na Korea Kusini

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais Donald Trump amesema Marekani itapunguza kwa kiasi kikubwa mazoezi ya kijeshi ya pamoja na Korea Kusini, akitaja "uhusiano wake mzuri sana" na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un.

    Pia aliangazia kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social hivi karibuni kwamba Korea Kusini ilikataa kuungana na Marekani katika mchakato wa kuiondolea Iran uwezo wa kumiliki silaha za nyuklia.

    "Mazoezi haya sio ya gharama kubwa tu—ambapo sehemu kubwa ya gharama hizo hulipwa na Marekani (kama kawaida!)—bali pia yanatoa ishara isiyofaa kabisa na ya uhasama," Trump aliandika.

    Seoul ilisema mazoezi hayo na Marekani yataendelea "kama ilivyopangwa". Pyongyang bado haijatoa tamko lolote. Haya yanajiri baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora yake ya balistiki mwezi huu, hatua ambayo imepigwa marufuku na Umoja wa Mataifa.

    Katika ujumbe wake wa mitandao ya kijamii siku ya Jumapili, Trump alisema ilikuwa "ni vigumu kuahirisha," mpango huo kwani Marekani na Korea Kusini zilikuwa zikitarajiwa kuanza mazoezi yao ya kila mwaka ya kijeshi Jumatatu.

    Walieleza kuwa zoezi hilo la siku 11 litakuwa na ukubwa sawa na lile ya miaka iliyopita, itahusisha takriban wanajeshi 18,000 wa Korea Kusini.

    Katika mkutano na waandishi wa habari, viongozi wa kijeshi pia walizungumzia hatua ya Korea Kaskazini kupeleka wanajeshi kusaidia vita vya Urusi dhidi ya Ukraine.

    Msemaji wa jeshi la Marekani, Ryan Donald, alisema "mafunzo yetu yanazingatia tishio hilo," akiashiria suala la wanajeshi wa Korea Kaskazini kurejea kutoka uwanja wa vita. Takriban wanajeshi 28,500 wa Marekani wamepelekwa nchini Korea Kusini.

    Soma zaidi:

  5. Mjumbe wa Trump akutana na kiongozi wa Hamas kushinikiza mpango wa amani Gaza

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mjumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump katika Mashariki ya Kati, Jared Kushner, amefanya mazungumzo nadra na Hamas kujadili utekelezaji wa mpango wa amani wa Gaza unaoungwa mkono na Marekani.

    Afisa mmoja wa Palestina ameiambia BBC kuwa mkwe wa Trump alikutana na ujumbe ulioongozwa na kiongozi mpya wa Hamas, Khalil al-Hayya, nchini Misri siku ya Jumapili.

    "Mwezi uliopita, Bodi ya Amani ya Trump ilisema kulikuwa na makubaliano ya Hamas na makundi mengine yenye silaha huko Gaza kuvuliwa silaha kabisa."

    Wiki iliyopita, Israel ilikataa mpango wa Trump wa vipengele 15 unaotaka jeshi la Israel kujiondoa Gaza na eneo hilo kujengwa upya chini ya uongozi mpya wa kiraia wa Wapalestina.

    Nchi nane za Kiislamu zilitoa taarifa siku ya Jumapili zikilaani uamuzi wa Israel wa kukataa mpango huo.

    Trump anaongoza Bodi ya Amani, shirika la kimataifa lililoanzishwa awali kwa lengo la kuleta amani Gaza, lakini baadaye likaongezewa jukumu la kushughulikia migogoro mbalimbali duniani.

    Inadaiwa kuwa mkutano kati ya Kushner na Hayya ni wa kwanza wa ngazi hiyo kufanyika tangu makubaliano ya usitishaji mapigano katika Ukanda wa Gaza yalipofikiwa mwaka jana.

    Soma Zaidi:

  6. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara 17/08/2026.