Israel yatangaza kudhibiti Kasri la Beaufort nchini Lebanon
Jeshi la Israel leo (Jumapili) limetangaza kuwa limekuwa likipanua operesheni zake za ardhini kusini mwa Lebanon, baada ya kuvuka Mto Litani, na kuashiria kuwa limechukua udhibiti wa Kasri ya Beaufort.
Msemaji wa jeshi Avichai Adraee aliandika kupitia jukwaa la X kwamba majeshi ya Israel yalivuka Mto Litani na kupanua mashambulizi yao dhidi ya Hezbollah kaskazini mwa mto huo, huku operesheni zikijumuisha maeneo ya ziada.
Adraee alisema kwamba alianzisha "operesheni kubwa katika Milima ya Shaqif na eneo la Wadi Saluki siku kadhaa zilizopita," kama sehemu ya "kuimarisha udhibiti wa operesheni kusini mwa Lebanon na kuondoa tishio la moja kwa moja dhidi ya Galilee Panhandle na mji wa Metula."
Amedokeza kuwa idadi kubwa ya wanajeshi wake wameanza mashambulizi "ili kupanua safu ya mbele ya ulinzi," na kuongeza kuwa vikosi vyake vinafanya kazi "karibu na Nabatieh, ambayo ni moja ya ngome kuu za kundi la kigaidi la Hezbollah kusini mwa Lebanon, na yuko tayari kuendelea na mashambulio akilazimika kufanya hivyo."
Wakati huo huo jeshi la Israel limetangaza kuwa limeshambulia miundo mbinu ya Hezbollah katika mji wa Tiro na maeneo mengine kusini mwa Lebanon.
Soma zaidi: