Ebola inasambaa kwa kiwango cha 'kutisha sana' DR Congo, MSF yaonya

Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images
Kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumezua hali ya "wasiwasi", shirika la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF) limeonya.
Akiongea wiki mbili baada ya mlipuko huo kutangazwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), naibu mkurugenzi wa MSF Dk Alan Gonzales alisema kamwe "kesi nyingi" hazijawahi kurekodiwa hivi karibuni.
Kauli yake inakuja wakati mkuu wa WHO Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus, alipotembelea mkoa wa Ituri mashariki mwa Congo - eneo lililoathiriwa zaidi - kuongoza harakati za kudhibiti virusi.
Takribani watu 246 wamefariki kutokana na ebola huku wengine zaidi ya 1,000 wakishukiwa kuwa na virusi ugonjwa huo.
Nchi jirani ya Uganda imeripoti kifo kimoja na kuthibitisha watu wameambukizwa.
"Wiki mbili baada ya kutangazwa kwa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Ituri, hali inazidi kuwa mbaya," Gonzalez alisema katika taarifa siku ya Jumamosi.
Ebola ni ugonjwa adimu lakini hatari unaosababishwa na virusi.
Virusi vya Ebola kwa kawaida huwapata wanyama, hasa popo, lakini binadamu huambukizwa wakati pale watu wanapokula au kushika wanyama walioambukizwa.
Huchukua siku mbili hadi 21 kwa dalili kujitokeza. Dalili huanza ghafla na kufanana na mafua, kama vile homa, maumivu ya kichwa, na uchovu.
Maelez zaidi:


