Waziri wa zamani nchini Tanzania ashauri Lissu aachiwe huru
Aliyekuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Anna Tibaijuka ametoa ushauri kwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani CHADEMA, Tundu Lissu aachiwe huru kwani kesi haikamiliki.
''Hekima na busara iliyokufanya kutangaza sera ya 4RS mara ulipoingia madarakani ikuongoze katika jambo hili''. Aliandika katika ukurasa wake wa X.
Amesema simulizi za kutisha za vyombo vya habari vya kimataifa, zinaibua hisia kali hasa kwa vijana, hata wazee wamekumbushwa kadhia ya operesheni sogeza iliyounda vijiji vya ujamaa mwaka 1974-1976.
Kitengo cha uchunguzi cha BBC Afrika Eye kimechapisha makala maalumu ya Tundu Lissu ikiwa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu kukamatwa kwake.
Lissu ambaye ni kiongozi wa upinzani nchini Tanzania, anakabiliwa na kesi ya uhaini.
Lissu, mwenye umri wa miaka 58, alikamatwa mwezi Aprili 2025 wakati akifanya kampeni chini ya kaulimbiu ya chama chake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), "Hakuna Mageuzi, Hakuna Uchaguzi."
Mamlaka zilielezea kuwa kampeni hiyo ilikuwa ikichochea umma kupinga kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Bi. Tibaijuka amesema kuwa taarifa hizi zinaathiri kikubwa taswira ya taifa la Tanzania na maslahi yake.
"Athari ni kubwa. Tutafute mufaka kupitia uwajibikaji na maridhiano. Tuwe na hofu ya Mungu na kutambua miujiza yake, mfano wa risasi16 kushindwa kukomesha uhai ingawa maumivu ni makubwa". Aliandika.
Unaweza kusoma;