Watu kadhaa wahofiwa kuuawa Nigeria
Raia kadhaa wanaripotiwa kuuawa baada ya ndege za Jeshi la Nigeria kufanya mashambulizi ya angani katika kijii kimoja kaskazini mashariki mwa nchi hiyo siku ya Jumamosi.
Kuna taarifa za kukinzana kuhusu idadi kamili ya watu waliouawa katika shambulizi hilo huku baadhi ya vyanzo vikiripoti kuwa zaidi ya watu 200 huenda waliuawa.
Eneo hilo liko mpakani kati ya majimbo ya Yobe na Borno ambako kundi la waasi la Boko Haram limekuwa likifanya uasi kwa muda mrefu.
Jeshi la Nigeria limesema lililenga maeneo yaliyo na magaidi lakini limeongeza kuwa litachunguza kilichojiri.
Kaskazini-mashariki mwa Nigeria kumeshuhudia matukio ya mara kwa mara katika miaka ya hivi karibuni ambapo operesheni za anga za kijeshi dhidi ya wanamgambo wenye itikadi kali.
Opereshine hizo zime zimewalenga kimakosa raia, ikiwa ni pamoja na vijijini, kambi za watu waliokimbia makazi na masoko.
Soma zaidi: