Moja kwa moja, Trump: Nimewaagiza wapatanishi kutoharakisha kufanya makubaliano na Iran

Makubaliano yanayojadiliwa yanaripotiwa kuhusisha kuongeza muda wa kusitisha mapigano hadi siku 60, kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz na mpango wa mazungumzo zaidi kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

Muhtasari

Trump asema hana 'haraka' kufanya makubaliano na Iran

Moja kwa moja

NaMariam Mjahid

  1. Mwanaanga wa China kuishi mwaka mzima anga za juu huku Beijing ikijipanga kuelekea Mwezini

    g

    Chanzo cha picha, CMSA/CCTV)

    China imezindua safari mpya ya anga za juu inayojumuisha watu watatu kuelekea kituo chake cha anga cha Tiangong Space Station, ambapo mmoja wa wanaanga hao atatumia mwaka mzima akiwa katika mzunguko wa Dunia.

    Hatua hiyo inachukuliwa kuwa sehemu muhimu ya maandalizi ya mpango wa Beijing wa kupeleka binadamu Mwezini ifikapo mwaka 2030.

    Misheni hiyo, inayojulikana kama Shenzhou-23, imezinduliwa siku ya Jumapili kwa kutumia roketi ya Long March 2F kutoka kituo cha kurushia vyombo vya anga cha Jiuquan kilichopo katika Jangwa la Gobi, kaskazini magharibi mwa China.

    Katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, China imewekeza mabilioni ya dola katika sekta ya anga huku ikilenga kujiimarisha kama moja ya mataifa yanayoongoza katika uchunguzi wa anga za juu.

    Tangu mwaka 2021, misheni za Shenzhou zimekuwa zikituma wanaanga watatu kwa wakati mmoja katika kituo cha Tiangong kwa safari za takribani miezi sita. Hata hivyo, safari hii itakuwa ya kipekee kwa kuwa itashuhudia mwanaanga mmoja akibaki angani kwa muda wa mwaka mzima kwa mara ya kwanza katika historia ya mpango wa anga wa China.

    Miongoni mwa wanaanga walioko katika misheni hiyo ni Li Jiaying mwenye umri wa miaka 43, ambaye amekuwa mwanaanga wa kwanza kutoka Hong Kong kushiriki katika safari ya anga. Kabla ya kujiunga na mpango wa anga wa China, Li aliwahi kufanya kazi katika jeshi la polisi la Hong Kong.

    Wanachama wengine wa misheni hio ni Zhu Yangzhu, mhandisi wa anga mwenye umri wa miaka 39, na Zhang Zhiyuan, mwenye umri wa miaka 39 na aliyekuwa rubani wa Jeshi la Anga la China. Kwa wote wawili, hii ni safari yao ya kwanza kwenda angani.

    Wakiwa katika kituo cha Tiangong, wanaanga hao wanatarajiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya kisayansi inayohusu sayansi ya maisha, sayansi ya vifaa, fizikia ya vimiminika na tiba.

    Jaribio muhimu zaidi katika misheni ya Shenzhou 23 ni kufuatilia athari za kukaa kwa muda mrefu katika mazingira yenye mvutano mdogo wa nguvu za uvutano yaani gravity. Utafiti huo unalenga kusaidia maandalizi ya safari za baadaye za kuelekea Mwezini na hata sayari ya Mirihi.

    Shirika la Anga la China limesema kuwa mwanaanga atakayechaguliwa kubaki angani kwa mwaka mmoja atatangazwa baadaye kulingana na maendeleo ya misheni hiyo.

    Mtaalamu wa unajimu na profesa katika Chuo Kikuu cha Macquarie nchini Australia, Richard de Grijs, amesema changamoto kuu za safari za muda mrefu angani ni pamoja na kupungua kwa msongamano wa mifupa, kudhoofika kwa misuli, kuathiriwa na mionzi ya anga, matatizo ya usingizi pamoja na uchovu wa kisaikolojia na kitabia.

    Ameongeza kuwa mifumo ya uhakika ya kuchakata maji na hewa, pamoja na uwezo wa kukabiliana na dharura za kiafya mbali na Dunia, ni mambo muhimu yatakayochangia mafanikio ya safari za muda mrefu za anga katika siku zijazo.

    Soma zaidi:

  2. Katika Picha: Jinsi Arsenali ilivyosherehea kukabidhiwa rasmi kombe la EPL 2026

    F

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Ilikuwa siku ya kipekee kwa kocha Mikel Arteta kuifurahia. Akiwa mbele ya mmiliki wa klabu, Stan Kroenke, ambaye alishuhudia mchezo huo akiwa uwanjani katika moja ya ziara zake nadra za kuifuatilia timu ana kwa ana, Arsenal walisherehekea ubingwa wao wa kwanza wa ligi tangu mwaka 2004 baada ya kuichapa kwa urahisi Crystal Palace.

    Arsenal walithibitisha ubora wao kwa ushindi huo muhimu, huku Crystal Palace wakionekana kuwa na mawazo zaidi kuelekea fainali yao ya michuano ya Ulaya inayowasubiri. Ushindi huo ulihitimisha safari ndefu ya kusaka taji la ligi na kuwapa Mashabiki wa Arsenal sababu ya kushangilia baada ya kusubiri kwa zaidi ya miongo miwili.

    F

    Chanzo cha picha, Getty Images

    G

    Chanzo cha picha, Getty Images

    F

    Chanzo cha picha, Getty Images

  3. Trump: Nimewaagiza wapatanishi kutoharakisha kufikia makubaliano na Iran

    g

    Chanzo cha picha, Afp via Getty

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema amewaagiza wapatanishi wa Marekani “kutoharakisha kufikia makubaliano” na Iran, baada ya hapo awali kuashiria kuwa pande hizo zilikuwa karibu kufikia mwafaka.

    Makubaliano yanayojadiliwa yanaripotiwa kujumuisha kuongezwa kwa usitishaji mapigano kwa siku 60, kufunguliwa tena kwa Mlango Bahari wa Hormuz, pamoja na mpango wa kuendelea na mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

    Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Trump alisema mazungumzo yanaendelea kwa “mtazamo chanya”, lakini akasisitiza kuwa:

    “Pande zote mbili zinapaswa kuchukua muda wao na kuhakikisha kila jambo linafanyika kwa usahihi.”

    Siku ya Jumamosi, Trump alisema kuwa makubaliano hayo yalikuwa “kwa kiasi kikubwa yamejadiliwa”, hali iliyozua matarajio kwamba tangazo rasmi lingeweza kutolewa wakati wowote.

    Kwa upande wake, maafisa wa Iran pia wameashiria kuwepo kwa maendeleo katika mazungumzo hayo. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, alisema kuwa pande hizo mbili ziko:

    “Karibu sana sio mbali sana” kufikia makubaliano.

    Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Marekani, makubaliano yanayojadiliwa kwa sasa si suluhisho la mwisho, bali yanaacha baadhi ya masuala magumu zaidi yaamuliwe katika mazungumzo ya baadaye.

    Masuala hayo ni pamoja na matakwa ya Iran ya kuondolewa vikwazo vya kiuchumi, kurejeshewa fedha zake zilizozuiwa nje ya nchi, pamoja na shinikizo la Washington kwa Iran kupunguza shughuli zake za nyuklia.

    Ripoti hizo pia zinasema kuwa mapendekezo ya makubaliano hayo yamezua mgawanyiko ndani ya Chama cha Republican, huku baadhi ya wanachama wakidai kuwa masharti yake yanaipa Iran nafuu kubwa kupita kiasi.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Hujambo na karibu kwa matangazo ya Jumatatu ya tarehe 25 mwezi Mei 2026.