Watu 16 wauawa katika shambulio la Urusi nchini Ukraine
Timu ya waokoaji nchini Ukraine, inaendelea kuwatafuta manusura katika duka moja la jumla lililoshambuliwa na ndege isiyo na rubani ya Urusi.
Kulingana na maafisa wa polisi, watu 16 wameuawa na wengine 130 kujeruhiwa katika kituo hicho cha kibiashara mjini Kryvyi Rih hapo jana. Watu tisa bado hawajulikani walipo.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amesema shambulio hilo “ni la kikatili” kwani lilitekelezwa kwa awamu mbili, awamu ya pili ikiwalenga wahudumu wa dharura waliokuwa wamefika katika eneo la mkasa.
Wakati huo huo, maafisa wa polisi wa eneo hilo wamesema angalau watu wawili zaidi wameuawa katika mashambulizi mengine ya Urusi yaliyofanyika mapema hii leo. Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema ililenga miundombinu ya uchukuzi na maghala ya Ukraine.
Mkuu wa utawala wa kijeshi wa eneo la Dnipropetrovsk, Oleksandr Hanzha, amesema watoto 23 ni miongoni mwa waliojeruhiwa katika shambulio la Ijumaa kwenye duka hilo la jumla la kibiashara.
Soma pia: