Iran yasema ina 'karata mpya' vita vikirejea, mazungumzo yakiwa shakani
Kadiri muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani, Israel na Iran unavyokaribia kuisha, bado hakuna uthibitisho wa mazungumzo zaidi ya amani.
Spika wa bunge la Iran aliandika kwenye mtandao wa X akisema kwamba Iran imekuwa "ikiandaa mkakati mpya kwa ajili ya uwanja wa vita" katika wiki mbili zilizopita na "haitakubali mazungumzo chini ya kivuli cha vitisho".
Wakati huo huo, Rais Donald Trump amekanusha kwamba yuko chini ya shinikizo la kufanya makubaliano, huku vyombo vya habari vya Marekani vikiripoti kwamba makamu wa rais JD Vance atasafiri kwenda Pakistan Jumanne kwa mazungumzo.
Katika Ghuba, Marekani inaendelea kuzuia Mlango wa Hormuz baada ya kukamata meli ya mizigo yenye bendera ya Iran siku ya Jumapili na pande zote mbili zinashutumiana kwa ukiukaji wa mapigano.
Kwingineko, duru ya pili ya mazungumzo kati ya Israeli na Lebanon inatarajiwa kufanyika Alhamisi kwa mujibu wa afisa wa Marekani.