Israel yapeleka wanajeshi zaidi katika kijiji ambako familia za Palestina zimezingirwa
Israel imesema itapeleka wanajeshi zaidi katika kijiji kimoja cha Ukingo wa Magharibi, ambako walowezi wa Kiyahudi wamezizingira familia mbili za Wapalestina ndani ya nyumba zao tangu Jumapili.
Video iliyotolewa inaonyesha kundi la kwanza la wanajeshi wa Israel likiingia katika eneo hilo, huku baadhi yao wakionekana kusali pamoja na wakazi wa Kiyahudi wenye misimamo mikali.
Maafisa zaidi wa usalama walipelekwa katika eneo hilo na kuondoa hema lililokuwa limewekwa hapo. Hata hivyo, waliondoka baada ya mapigano kuzuka, na wakazi kurejea katika eneo hilo.
Familia za Wapalestina zinazoishi katika kijiji cha Qasra, kusini mwa Nablus, zimesema zimekatiliwa huduma za maji na umeme, huku akiba yao ya chakula ikizidi kupungua.
Kwa mujibu wa sheria za kimataifa, makazi yote ya Wayahudi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel ni kinyume cha sheria.
Soma Zaidi: