Mamia ya raia wa kigeni bado hawajulikani walipo katika eneo la mpaka Nepal

Chanzo cha picha, RSS
Watalii kutoka kote duniani huja Nepal kwa ajili ya milima na maeneo yake matakatifu.
Taarifa kuhusu watu hao waliopotea ni kama ifuatavyo:
- India - Takriban raia 320 wa India hawajulikani walipo, kulingana na wizara ya mambo ya nje mjini Delhi
- China - Wizara ya mambo ya nje ya China inasema karibu raia 100 wa China hawajulikani walipo nchini Nepal
- Marekani - Wamarekani 90 bado hawajulikani walipo, kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani
- Ukraine - Raia 62 wa Ukraine hawajulikani walipo, polisi wa Nepal wanasema
- Malaysia - Raia 51 wa Malaysia waliokuwa wakisafiri na kampuni ya Fishtail Tours and Travels hawajulikani walipo kufuatia mafuriko, maafisa wanasema
- Australia - Hakuna taarifa kuhusu walipo raia 41 wa Australia, kulingana na naibu waziri wa uhamiaji wa nchi hiyo
- Uingereza - Polisi wa Nepal wanasema raia 33 wa Uingereza hawajulikani walipo; shirika la utangazaji la serikali ya China, CCTV, pia linaripoti kuwa raia 15 wa Uingereza ni miongoni mwa waliopotea huko Tibet - haijulikani ni wangapi kati yao ambao tayari wamejumuishwa katika takwimu zilizotolewa na Nepal
- Canada - raia 30 wa Canada hawajulikani walipo, wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo inasema
- Idadi ndogo ya wasafiri kutoka Korea Kusini, Afrika Kusini, Ureno, Uholanzi na New Zealand pia ni miongoni mwa waliopotea.


