Moja kwa moja, Iran yatishia kushambulia nchi itakayoisaidia Marekani

Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Iran, Mohsen Rezaei, amesema "nchi yoyote itakayoisaidia Marekani kutekeleza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya nchi yetu inachukuliwa kuwa adui."

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Iran yatishia kushambulia nchi itakayoisaidia Marekani

    Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Iran, Mohsen Rezaei, amesema kwamba "nchi yoyote itakayoisaidia Marekani kutekeleza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya nchi yetu inachukuliwa kuwa adui."

    Rezaei aliongeza katika taarifa kwa televisheni ya taifa: "Tunaziarifu nchi jirani na nchi zingine duniani: Msijiunge na vita vya kiuchumi vinavyoendeshwa na Marekani."

    "Maslahi ya nchi zinazosaidia Marekani kuendesha vita vya kiuchumi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu italengwa," alisema Rezaei, na kuongeza: "Kwa nchi jirani zitashirikiana na Wamarekani katika vita hivyo vya kiuchumi, hakuna tone hata moja la mafuta litakalotoka..." Ghuba na Lango la Hormuz.

    Kauli ya Rezaei inakuja baada ya Washington kutangaza kuwa itaimarisha vikwazo vya kiuchumi ili kuishinikiza Tehran kurejea kwenye meza ya mazungumzo.

    Rezaei aliendelea kusema: "Bado hatujashambulia maslahi yoyote ya kiuchumi ya Marekani, mpaka sasa tumelenga kambi za kijeshi tu; lakini iwapo wanataka kutuwekea vikwazo vya kiuchumi, basi kampuni za mafuta na za kiuchumi za Marekani zilizo karibu na Iran na maeneo mengine, zijiandae kwa mapigo yetu ."

    Soma pia:

  2. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja.