Baraza la amani Gaza laonya Hamas kuhusu kuchochea vita
Baraza linalosimamia amani eneo la Gaza, linaloongozwa na Marekani, limeionya Hamas dhidi ya kurusha tiara au ndege za karatasi, baada ya Israel kutishia kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi.
“Shughuli zozote za kijeshi huko Gaza lazima zisitishwe, ikiwemo kurusha ndege za karatasi,” afisa mmoja wa Baraza la Amani, ambaye hakutaka kutajwa jina, alisema. “Tumewasilisha ujumbe huu moja kwa moja kupitia utaratibu uliopo.”
Aliongezea kuwa “Israel nayo lazima iheshimu usitishaji mapigano.”
Ndege za karatasi zilizorushwa kutoka Ukanda wa Gaza siku za hivi karibuni zimeongeza tena mvutano katika maeneo yanayopakana na Gaza.
Kulingana na vyombo vya habari vya Israel, takriban ndege 10 za karatasi zimepatikana au kuzuiwa katika siku za hivi karibuni, huku Israel pia ikiripoti kurusha ndege zisizo na rubani.
Hamas imekanusha kuhusika na urushaji wa ndege hizo za karatasi, ikisema watoto walioko Gaza ndio waliozirusha.
Shirika la Utangazaji la Israel, Kan, lilinukuu jeshi la Israel lilolosema kuwa ndege hizo zilizopatikana hazikuwa na vilipuzi wala vitu vya kutiliwa shaka.
Soma pia: