Vance: Trump hana nia ya kuishambulia tena Iran bila sababu za msingi
Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, amesema Rais Donald Trump hana nia ya kuanzisha tena operesheni za kijeshi dhidi ya Iran bila kuwa na lengo lililo wazi na maalumu.
Akizungumza na waandishi wa habari Jumatano, Vance alisema, "Ninachoweza kuthibitisha ni kwamba Rais Trump hana nia ya kuwarejesha wanajeshi wetu huko isipokuwa pale ambapo itakuwa lazima kabisa kufanya hivyo."
Makamu huyo wa Rais alionya kuwa jaribio lolote la Iran kufufua mpango wake wa nyuklia au kuhatarisha usafirishaji wa kibiashara baharini linaweza kuilazimisha Washington kubadili mkakati wake.
Vance pia alithibitisha kuwa mazungumzo yanayoendelea mjini Doha "yanapiga hatua vizuri" na kusisitiza kuwa utawala wa Marekani unaendelea kushiriki katika mazungumzo hayo "kwa nia njema."
Unaweza kusoma;