Moja kwa moja, Marekani na Iran zashambuliana kwa siku ya pili,afisa mkuu wa Iran asema "kukiuka makubaliano kutakuwa"na gharama

Marekani imeanzisha wimbi jipya la mashambulizi ya anga dhidi ya Iran, huku milipuko ikiripotiwa katika maeneo ya kusini mwa nchi, ikiwemo karibu na Bandar Abbas na maeneo mengine ya pwani.

Skip Video and continue reading
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

  1. Rais wa Nigeria ataka kujua jinsi taasisi feki ilivyoanzishwa ndani ya ofisi yake

    Rais Tinubu

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, ameagiza kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za ufisadi baada ya madai kwamba taasisi ya serikali isiyokuwepo kisheria iliundwa ndani ya ofisi yake na kupewa fedha za umma zenye thamani ya dola za Marekani 950,000.

    Kwa mujibu wa Ikulu ya Nigeria, barua iliyodaiwa kutolewa na Mkuu wa Wafanyakazi wa Rais ya kuanzisha Presidential Foreign Intervention Promotion Council (PFIPC) ilikuwa ya kughushi.

    Polisi wameanzisha msako dhidi ya Adeniyi Adeyemi Matthew, ambaye alikuwa akijitambulisha kama Mkurugenzi Mkuu wa PFIPC, kwa tuhuma za kughushi nyaraka, kujifanya afisa wa umma na makosa mengine yanayohusiana.

    Kabla ya kutoweka, Adeyemi aliviambia vyombo vya habari vya nchini humo kuwa hana hatia na kwamba ana hofu kuhusu usalama wa maisha yake.

    Aliahidi kufika mahakamani kuthibitisha kutokuwa na hatia, akisisitiza kuwa taasisi hiyo ilianzishwa kwa mujibu wa sheria. Pia aliwashutumu baadhi ya maafisa waandamizi serikalini kwa kudai rushwa wakati wa mchakato wa uteuzi wake na baadaye kujaribu kudhibiti fedha za taasisi hiyo. Ikulu imekanusha tuhuma hizo.

    Adeyemi alisema PFIPC ilianzishwa mwaka 2024 kwa lengo la kuvutia uwekezaji wa kigeni nchini Nigeria, lakini hakuna rekodi yoyote inayoonesha kuwa ilifanikiwa kufanikisha uwekezaji wowote.

    Taasisi hiyo ina wafanyakazi watatu pekee, ambao tayari wamehojiwa na polisi.

    Jumanne, Rais Tinubu aliiagiza Tume Huru ya kupambana na vitendo vya rushwa (ICPC) kufanya uchunguzi na kuwasilisha ripoti kamili ndani ya siku 30.

    Uchunguzi wa BBC News Pidgin umebaini kuwa taasisi hiyo ilikuwa imepata ofisi ndani ya Federal Secretariat, jengo kubwa la serikali linalohifadhi wizara nyingi za Nigeria katika mji mkuu, Abuja.

    Pia ilifungua akaunti za benki katika Benki Kuu ya Nigeria (CBN) na iliorodheshwa katika Sheria ya Bajeti ya mwaka 2026 ikiwa na mgao wa naira bilioni 1.3, sawa na dola za Marekani 950,000.

    Hata hivyo, Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali imesema PFIPC haikuwahi kuwa na akaunti inayofanya kazi katika Benki Kuu ya Nigeria, na haijawahi kupokea fedha za umma wala kulipa mishahara.

    Ikulu ya Rais imesema uchunguzi wa kisayansi uliofanywa na polisi umethibitisha kuwa saini ya Mkuu wa Wafanyakazi wa Rais, Femi Gbajabiamila, iliyokuwa kwenye barua inayodaiwa kuanzisha taasisi hiyo, ilighushiwa.

    Kwa mujibu wa mashtaka yaliyowasilishwa katika Mahakama Kuu, mjini Abuja, Adeniyi Adeyemi pamoja na washtakiwa wengine wawili wanatuhumiwa kutumia nyaraka za serikali zilizoghushiwa kuanzisha na kuendesha taasisi hiyo inayodaiwa kuwapo, kufungua akaunti kadhaa za benki kwa jina lake na kutafuta kutambuliwa rasmi kwa taasisi ambayo serikali inasisitiza kuwa haipo.

    Rais Bola Tinubu ameiagiza Tume Huru ya Kupambana na Vitendo vya Rushwa na Makosa Mengine Yanayohusiana (ICPC) kuchunguza tuhuma mbalimbali, zikiwemo:

    • Kughushi barua za uteuzi na nyaraka rasmi za serikali;
    • Kutumia madai ya uongo kutafuta utambuzi rasmi na uungwaji mkono wa kidiplomasia, ikiwemo kuwezesha upatikanaji wa visa;
    • Kufungua akaunti nyingi za benki kwa kutumia nyaraka zinazodaiwa kughushiwa; na
    • Kuchunguza nafasi ya mtumishi yeyote wa umma, mtu binafsi, taasisi ya kifedha au mpatanishi ambaye huenda alihusika katika kuwezesha njama hiyo.

    Rais pia ameagiza wachunguzi kuchunguza mazingira yaliyoifanya taasisi inayodaiwa kuwa ya kubuniwa ionekane kuwa halali, pamoja na kubaini udhaifu katika mifumo na taratibu za serikali ambao unadaiwa kutumiwa kufanikisha mpango huo.

    Kashfa hiyo imezua shinikizo kubwa kutoka kwa mashirika ya kiraia, wanasiasa wa upinzani na mawakili waandamizi, ambao wamekuwa wakitaka kufanyika kwa uchunguzi huru kuhusu suala hilo.

  2. Mahakama ya ICC imesema imepata ushahidi katika uchunguzi wa uhalifu wa kivita nchini Sudan

    Makumi ya maelfu ya watu walikimbia mji wa El-Fasher baada ya kutwaliwa na kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF).

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Maelezo ya picha, Makumi ya maelfu ya watu walikimbia mji wa El-Fasher baada ya kutwaliwa na kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF).

    Naibu Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), Nazhat Shameem Khan, amesema mahakama hiyo imepata "ushahidi thabiti" unaowahusisha viongozi wa kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF) na uhalifu wa kivita uliofanyika hivi karibuni katika jimbo la Darfur, Sudan.

    Akizungumza na BBC, Khan alisema ICC imepata "mafanikio makubwa" katika uchunguzi wake kuhusu mauaji ya raia yaliyotokea katika miji ya El-Fasher na El-Geneina.

    "Huenda ikachukua muda kabla haki haijapatikana na kesi kufikishwa mahakamani, lakini tutafika huko," alisema Khan, akiongeza kuwa ushahidi pia unawahusisha viongozi wa RSF na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

    Kuzingirwa na hatimaye kutwaliwa kwa mji wa El-Fasher kulikuwa miongoni mwa matukio mabaya zaidi katika vita vinavyoendelea kati ya RSF na jeshi la Sudan.

    Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 6,000 waliuawa mjini El-Fasher wakati RSF ilipouteka mji huo mwezi Oktoba mwaka jana.

    Aidha, kikundi hicho kinatuhumiwa kutekeleza mauaji ya halaiki kama hayo katika mji wa El-Geneina.

    RSF imeendelea kukanusha mara kwa mara tuhuma za kuhusika na mauaji ya watu wengi katika eneo lolote la Darfur.

    Hata hivyo, hakutaja ni lini mashtaka yanaweza kufunguliwa dhidi ya wale wanaodaiwa kuhusika na ukatili uliotekelezwa katika vita hivyo, vilivyoanza mwezi Aprili 2023.

    Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), yenye makao yake makuu mjini The Hague nchini Uholanzi, ni mahakama ya kimataifa yenye mamlaka ya kushtaki watu wanaotuhumiwa kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita.

    Khan alizungumza na BBC baada ya kutembelea kambi za wakimbizi mashariki mwa Chad, ambako watu waliokimbia mapigano huko Darfur walimweleza kuhusu ukatili walioupitia.

    Makumi ya maelfu ya watu walilazimika kuyahama makazi yao mjini El-Fasher, huku Umoja wa Mataifa ukisema kuwa ghasia zilizotokea huko zilikuwa na "viashiria vya mauaji ya kimbari."

    RSF imekanusha madai yaliyoenea kwamba mauaji yaliyotokea El-Fasher yalichochewa na misingi ya kikabila na kwamba yalifuata mtindo wa wanamgambo Waarabu kuwashambulia makundi yasiyo ya Kiarabu.

    Kikundi hicho kimesisitiza kuwa kiwango cha ukatili kilichoripotiwa kimezidishwa, ingawa kimekiri kwamba baadhi ya ukiukaji wa haki za binadamu ulitokea katika mji huo.

    Unaweza kusoma;

  3. Marekani yaanzisha mashambulizi zaidi dhidi ya Iran huku milipuko ikiripotiwa kusini mwa nchi

    Milipuko kadhaa iliripotiwa katika maeneo mbalimbali ya pwani ya Iran, ikiwemo miji ya Konarak na Chabahar.

    Chanzo cha picha, Reuters

    Marekani imeanzisha wimbi jipya la mashambulizi ya anga dhidi ya Iran, huku milipuko ikiripotiwa katika maeneo ya kusini mwa nchi, ikiwemo karibu na Bandar Abbas na maeneo mengine ya pwani.

    Maafisa wa Marekani wamesema mashambulizi hayo yanalenga kupunguza uwezo wa Iran wa kutishia usafiri wa majini katika Mlango bahari wa Hormuz, kufuatia mashambulizi yaliyodaiwa kufanywa na Iran dhidi ya meli za kibiashara.

    Iran imekosoa mashambulizi hayo na kuyataja kuwa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano, huku ikidai kujibu kwa kushambulia vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Ghuba.

    Mvutano huo umeongeza hofu ya kuenea kwa mzozo katika Mashariki ya Kati na kusababisha bei za mafuta kupanda katika masoko ya dunia.

    Milipuko kadhaa iliripotiwa katika maeneo mbalimbali ya pwani ya Iran, ikiwemo miji ya Konarak na Chabahar.

    Televisheni ya taifa ya Iran imeripoti kuwa milipuko minane imetokea katika mji wa Bandar Abbas, huku ikidai kwamba makombora mawili yalipiga bandari za Sirik na Jask, ambazo zote ziko kusini mwa Iran.

    Vyombo vya habari vya serikali pia vilisema kuwa makombora mawili yalilipiga kisiwa cha Abu Musa, eneo ambalo limekuwa likizozaniwa umiliki kwa muda mrefu kati ya Iran na Falme za Kiarabu.

    Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari vya serikali ya Iran, mifumo ya ulinzi wa anga imewashwa katika mji wa Bandar Abbas kufuatia mashambulizi hayo.

    Kiwango halisi cha uharibifu uliosababishwa na mashambulizi ya Marekani bado hakijajulikana. Hata hivyo, vyombo vya habari vya Iran vimeripoti kukatika kwa umeme katika mji wa Chabahar na kuzuka kwa moto katika kambi ya Jeshi la Iran mjini Bushehr.

    Akizungumza na waandishi wa habari akiwa ndani ya ndege ya rais, Air Force One, Jumatano jioni, Rais Donald Trump alisema Iran ilikuwa imewasiliana na Marekani muda mfupi uliopita na ilikuwa "inataka kufikia makubaliano kwa udi na uvumba."

    Trump aliongeza: "Sijui kama wanafaa kufanya makubaliano. Sijui kama watayaheshimu makubaliano hayo, hilo ndilo tatizo."

    Unaweza kusoma;

  4. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu za leo