Licha ya kutoka sare ushindi nyumbani dhidi ya Manchester City waliopata bao la kusawazisha la dakika za jioni kupitia Erling Haaland, Bournemouth bado wameandika historia kubwa kwa kufuzu michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo.
Sare ya bao 1-1 dhidi ya City katika Uwanja wa Vitality usiku wa Jumanne imeihakikishia Bournemouth nafasi ya kushiriki michuano ya Europa League msimu ujao.
Hata hivyo, bado kuna uwezekano kwa Bournemouth kufuzu hadi Ligi ya Mabingwa Ulaya kulingana na matokeo ya mechi za mwisho za msimu.
Iwapo Aston Villa wataifunga Freiburg katika fainali ya Europa League itakayochezwa Jumatano usiku, Bournemouth kuna uwezekano ku kupata nafasi hiyo.
Villa wakitwaa ubingwa huo na kumaliza nafasi ya tano kwenye msimamo wa EPL, watapata tiketi ya moja kwa moja ya Ligi ya mabingwa League kama mabingwa wa Europa League.
Hivyo itafanya nafasi ya ziada ya timu ya Ligi kuu England (EPL) kwenda kwa timu itakayomaliza nafasi ya sita, jambo ambalo linaweza kuinufaisha Bournemouth.
Ili hilo litokee, Aston Villa wanapaswa kupoteza dhidi ya Manchester City huku Liverpool wakishinda nyumbani dhidi ya Brentford.
Kwa upande wa Bournemouth, watakuwa na uhakika wa kumaliza nafasi ya sita iwapo wataepuka kupoteza dhidi ya Nottingham Forest au Brighton wakashindwa kuifunga Manchester United.
Bado kuna uwezekano mwingine mdogo wa Bournemouth kufuzu Ligi ya mabingwa Ulaya ikiwa Liverpool watapoteza kwa kipigo kikubwa katika mchezo wao wa mwisho huku Bournemouth wakishinda kwa mabao mengi.
Kwa mfano, Liverpool wakifungwa mabao 3-0 na Bournemouth kushinda 4-0, tofauti ya mabao inaweza kuibeba Bournemouth.
Pia njia ya kipekee zaidi inaweza kutokea ikiwa Liverpool wakifungwa 1-0 na Bournemouth kushinda 5-0.
Katika mazingira hayo, timu hizo zinaweza kuwa sawa kwa kila kitu hadi kuhitaji mechi ya mchujo maalum ya mwisho wa msimu kuamua nani afuzu ligi ya mabingwa.
Wakati Arsenal tayari wametwaa ubingwa wa EPL kwa mara ya kwanza baada ya miaka 22, bado kuna ushindani mkubwa katika michezo ya mwisho ya msimu huku nafasi za kufuzu mashindano ya Ulaya pamoja na vita vya kushuka daraja vikiwa bado havijaamuliwa.
Katika vita vya kushuka daraja, West Ham wanahitaji ushindi dhidi ya Leeds United ili kujiweka kwenye nafasi ya kuendelea kubaki EPL.
Tottenham pia wako kwenye presha kubwa huku wakihitaji ushindi dhidi ya Everton ili kuhakikisha hawashuki daraja.
Chelsea, Brighton, Brentford na Sunderland nazo bado zinapambana kuwania nafasi za michuano ya Ulaya kabla ya pazia la msimu kufungwa rasmi Jumapili hii.