Baadhi ya wanazuoni wa Iran watoa fatwa ya kutaka kuuawa kwa Trump na Netanyahu
Mgawanyiko usio wa kawaida umeripotiwa ndani ya Baraza la Wataalamu wa Iran, chombo cha juu zaidi cha wanazuoni wa kidini nchini humo.
Takriban theluthi mbili ya wajumbe wa baraza hilo lenye wanachama 88 walitoa fatwa ya kidini inayotaka kuuawa kwa Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.
Fatwa hiyo ilieleza kuwa ni wajibu wa Waislamu kuwaua viongozi hao wawili iwapo watapata fursa ya kufanya hivyo.
Hata hivyo, uongozi wa Baraza la Wataalamu umeitaja fatwa hiyo kuwa "isiyo ya kawaida", ukisema maudhui yake yanahitaji mjadala na uchambuzi zaidi.
Fatwa hiyo, iliyotolewa na wanazuoni wenye misimamo mikali, ilijumuishwa katika barua iliyotumwa kwa umma wa Iran.
Barua hiyo pia ilisema kuwa Tehran haipaswi kukubali kufunguliwa kwa Mlango wa Hormuz wala kujadili mpango wake wa nyuklia katika mazungumzo na Marekani.
Maelezo zaidi: