Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Vurugu Nigeria: Mashuhuda wa mauaji Nigeria wadai ‘polisi waliwapiga risasi’
Iliyochapishwa
Watu kadhaa wameripotiwa kupigwa risasi na kuuawa ama kujeruhiwa katika maandamano ya kupinga ukatili wa polisi mjini Lagos.
Walioshuhudia tukio hilo wameiambia BBC ilionekana 'kama vita' na kuongeza kwamba maandamano hayo yalikuwa ya amani lakini wanajeshi waliwapiga risasi kwa lengo la kuwaua.
Jeshi la Nigeria limekana kuhusika na mauaji hayo. Mashuhuda waliozungumza na BBC hawakujitambulisha kwa kuhofia usalama wao.