Mataifa 10 yanayoongoza katika uzalishaji wa mafuta duniani

Chanzo cha picha, Getty Images
Baada ya makubaliano ya kusitisha vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kwa wiki mbili yakianza kutekelezwa, mataifa yanayozalisha mafuta yameanza kupata umaarufu kwani yamegeuka kuwa tegemeo la mataifa mengi.
Changamoto ya uhaba wa mafuta imejiri baada ya mlango bahari wa Hormuz ambao husafirisha 20% ya mafuta yote duniani kufungwa.
Hii imesababisha bei ya mafuta kupanda, haswa mafuta yanayopitia mlango wa Hormuz. Sasa pipa moja la mafuta ghafi imefika dola 120.
Tunaangazia mataifa 10 yenye uzalishaji mkubwa wa mafuta ghafi.
Marekani- Mapipa milioni 22
Kwa zaidi ya miaka saba mfulululizo, Marekani imekuwa ikiongoza katika uzalishaji wa mafuta, na huzalisha zaidi ya mapipa millioni 22 kila siku.
Marekani pia ndiyo watumizi wakubwa wa mafuta ghafi, kutokana na idadi yake kubwa ya watu.
Jimbo la Texas ndilo linaloongoza katika uzalishaji wa mafuta.
Saudi Arabia- Mapipa millioni 10

Chanzo cha picha, Reuters
Saudi Arabia husambaza 17% ya mafuta kote duniani na pia inahifadhi kubwa ya mafuta.
Taifa hilo pia ndiyo muuzaji mkubwa wa mafuta katika masoko ya kimataifa na huzalisha mapipa millioni 10.88 kila siku.
Vita vinavyoendelea nchini Iran, vimeilazimu Saudi Arabia kupunguza uzalishaji wake wa mafuta kutoka mapipa million 10 hadi 8, baada ya kufungwa kwa mlango bahari wa Hormuz, ambayo ndiyo njia kuu ya kusafirisha mafuta kwa masoko ya nje.
Urusi- Mapipa million 10
Urusi huzalisha zaidi ya mapipa millioni 10 kwa siku, mafuta hayo yakipatikana magharibi mwa Serbia.
Shughuli zake za kuchimba mafuta zimeathirika baada ya vita vyake na Urusi, na mataifa mengi ya Ulaya na G7 kuwaekea vikwazo vya kuuza mafuta yake katika masoko ya kimataifa.
Kabla vita kuanza 2021, mataifa ya ulaya yalikuwa yakinunua 20% ya mafuta ya Urusi.
China na India ndiyo wanunuzi wakuu wa mafuta ya Urusi.
Canada – Mapipa millioni 5
Mwaka wa 2024, uzalishaji wa mafuta nchini Canada ulikuwa unakaribia mapipa millioni 6 kwa siku.
Mafuta hayo mengi huchimbwa katika wilaya ya Alberta.
Canada huuza mafuta yake mengi nchini Marekani.
China- Mapipa million 5
Kulingana na takwimu zilizochapishwa mwaka wa 2024, China huzalisha mapipa millioni 5.33 ya mafuta kila siku.
China ndiyo taifa la pili duniani ambalo hutumia mafuta ghafi kwa wingi.
Kutokana na idadi yake kubwa ya watu, China imekuwa taifa ambalo inatumia nishati nyingi kwa siku duniani, na huagiza mapipa million 11 ya mafuta kwa siku.
70% ya mafuta ya China hutoka Saudi Arabia na Iraq.
Iran- Mapipa million 4.5
Iran ni taifa la sita katika ukubwa wa uzalishaji wa mafuta.
Taifa hilo huzalisha takriban mapipa millioni 4.62 kwa siku kulingana na takwimu za 2024.
Kulingana na mamlaka ya nishati duniani EIA, Iran ina hifadhi kubwa ya mafuta ghafi duniani.
Iran huuza takriban mapipa millioni 1.4 kwa China, na hatua ya taifa hilo kufunga mlango bahari wa Hormuz kumeathiri bei ya mafuta duniani.
UAE- Mapipa million 4.5
Zaidi ya mwongo mmoja, UAE imekuwa miongoni mwa mataifa kumi yenye uzalishaji mkubwa wa mafuta, na huzalisha mapipa millioni 4.51 kila siku.
Taifa hilo linahifadhi kubwa ya mafuta ya hadi mapipa billioni 111, na mafuta mengi ya ardhini yakiwa mjini Abu Dhabi.
Taifa hilo hivi karibuni limepunguza uzalishaji wake wa mafuta, baada ya makombora ya Iran kulenga vituo vyake vya kuzalisha mafuta.
Iraq- Mapipa million 4.5
Iraq huzalisha mapipa millioni 4.4 kwa siku kulingana na takwimu za 2024.
Iraq pipa inahifadhi kubwa ya mafuta ambayo ni 11% ya mafuta duniani, kwa mapipa billioni 145.2.
Taifa hilo pia limeathirika na vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran.
Brazil- Mapipa million 4
Mwaka wa 2024, Brazil ilikuwa inazalisha mapipa millioni 4.28.
Brazil inatarajiwa kuwa miongoni mwa mataifa tano duniani yenye uzalishaji mkubwa wa mafuta katika siku za usoni.
Kuwait- Mapipa million 2.78
Kuwait huzalisha mapipa millioni 2.78 kila siku. Taifa hilo limeshindwa kuongeza uzalishaji wake na kurejelea viwango vya kawaida vya mapipa millioni 3.5, kutokana na hali ya kisiasa nchini humo.
Imetafsiriwa na Beldeen Waliaula












